gossips

Vidosho kutoka Uganda, Tanzania wafurika Rift Valley kukamua wazee bonasi ya chai

Mapenzi ya Utapezi, ni sura ya maisha halisi katika maeneo ya Bomet, Kericho, Kisii, Nandi, na Mlima Elgon huku wakulima wa chai wakianza kupokea bonasi kuanzia wiki hii.

Vidosho wanazidi kumiminika mjini Kericho, tayari kushiriki katika kazi ngumu ya wakulima hao.

Mikahawa ambayo kwa muda ilikuwa haipati wateja wengi, sasa imejaa watu, na magari kwenye barabara zinazoenda Kisii na Kericho zinapandisha viwango vya nauli.

Kwa wenyeji wa eneo hili, hii ni hali ya kawaida ambapo wanaona kuwa warembo kutoka nchi jirani za Tanzania na Uganda pia wamejiunga na wenzao wa Kenya kwenye mavuno.

Kwa upande mwingine, wakazi wa eneo la Konoin, Kaunti ya Bomet, wanalalamika kuhusu kuongezeka kwa maharamia wa mapenzi na kusema kuwa wanaume wanakumbwa na mitego mingi na kunyang’anywa mali zao.

“Badala ya kukodisha vyumba vya kulala nje ya mji, wanawapangishia karibu na maeneo yetu ili kuwadhibiti wanaume kwa muda mrefu na kuwapora kila kitu,” anasema Bi. Ann Chebet, muuzaji wa mananasi kwenye eneo la Ngoina Road.

Hata hivyo, katika kituo cha biashara cha Mogosiek, wakati huu wa msimu wa mavuno, vyumba vya kulala huwa vimejaa sana na wakazi wanahitajika kutumia vichaka kwa kukosa nafasi.

“Makahaba wachanga na wale wenye umri mkubwa hufika hapa mapema na kukodisha vyumba na kisha huwaleta wateja wao,” anasema Robert Kipkemoi, mkazi wa Mogogosiek.

Zaidi ya hayo, wamiliki wa baa na mikahawa wametajirika kutokana na mazingira mazuri ya kufanyia biashara na wanatarajia kuwa na idadi kubwa ya wateja.

Kipkemboi anasema kuwa hii imekuwa changamoto kwa familia nyingi katika eneo hili.

Tukumbuke kuwa Konoin ni eneo ambalo wengi wa wakulima wa chai hutoka katika Kaunti ya Bomet.